top of page

IS walipua madhabahu Syria

  • Writer: sembula
    sembula
  • Aug 31, 2015
  • 1 min read

Wapiganaji wa dola ya kiislamu IS, wanadaiwa kulipua sehemu ya madhabahu ya kidini katika mji wa Syria wa Palmyra.

Kundi la kutetea haki za binadamu nchini Syria limesema kuwa wanamgambo hao wametumia mabomu kulipua hekalu ya kiroma ya Bel.

Image captionMadhabahu yakilipuliwa

Shirika hilo limesema kuwa uharibifu mkubwa umetokea baadha ya shambulio hilo.

Wiki iliyopita wanamgambo hao wameoneshwa aktika video wakilipua hekalu nyingine ya kale ya Baalshamin. Islamic State waliuteka mji wa Palmyra mwezi Mei na kuzua hofu ya kushambuliwa madhabahu hayo.


 
 
 

Comments


RECENT POSTS:
SEARCH BY TAGS:

© 2023 by NOMAD ON THE ROAD. Proudly created with Wix.com

  • b-facebook
  • Twitter Round
  • Instagram Black Round
bottom of page