top of page

Nkurunziza atoa wito kupambana na mauaji

  • Writer: sembula
    sembula
  • Aug 27, 2015
  • 1 min read

Katika hotuba kwa taifa rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ameonyesha hisia zake kuhusu kujumuisha vikosi vya usalama nchini humo.

Hayo yamekuja wiki moja baada ya kuapishwa kushika hatamu za uongozi wa nchi hiyo ambapo wakasoaji wanasema ni kinyume cha katiba.

Suala hilo limezusha ghasia kali na jaribio lililotibuka la kuipindua serikali.

Amezitaka kamati za usalama kufanya kazi usiku na mchana kupambana kile alichokiita kundi la watu wachache wanaofanya mauaji na kusababisha hofu kwa raia.

Amesema vijana hasa wa vyuo vikuu sasa watapata mafunzo ya uzalendo.


 
 
 

Comments


RECENT POSTS:
SEARCH BY TAGS:

© 2023 by NOMAD ON THE ROAD. Proudly created with Wix.com

  • b-facebook
  • Twitter Round
  • Instagram Black Round
bottom of page